Saturday, September 22, 2012

"He Wants Your All" Young Adult Congress: 28-18/09/2012


The Southern New England Conference will be hosting a Young Adult/Collegiate Summit on September 28 and 29 at Atlantic Union College.

For more information visit: http://www.snecyouth.org/node/460

Impact Boston: 22 - 23 September 2012


Hope for Humanity Symposium:17-28 September 2012

Dear all,

You are all invited to the Better Living Symposium-HOPE FOR HUMANITY AMID GLOBAL CHALLENGES- currently going on at NSSF Water Front Conference room (8th Floor), Dar es Salaam (17 - 28 September 2012: 5 - 7pm)

There are presentations on issues facing our society both on secular and Holy books perspectives.

Come, learn and share your ideas with others

For more information see the attached bronchure!

SOURCE: THISDASO ASSOCIATES

Satellite Evangelism with Pastor Ruguri from 29/09/2012

The “Gospel Flame” Bible Lecture series with Pastor Ruguri coming from Kampala Uganda and being broadcast for Africa [from 29 September to 15 October 2012] will feature the power filled dynamic preaching of Blasious Ruguri. Pastor Ruguri has lectured and preached widely in many countries in Africa and North America. The series will also feature health and family talks and a remarkable wide range of gospel music from choirs from all across east – central Africa. The series is translated into seven languages with home viewers able to select the language of their choice.  English, Swahili, French and other major languages of Africa will be available.

Anyone with a Free To Air satellite system tuned to Intel Sat 10/20 will be able to share in the programs. The series will be available on both Ku (small dish) and C-band (big dish) reception. Millions of homes across Africa will be able to watch the programs. Nearly 10,000 Seventh-day Adventist Churches across Africa are also hosting the event for large local audiences.  

Reception parameter information for the small dish (Ku band) receivers is:

Hope Channel International [English]
Languages 1 to 7
Satellite: IS-10 Ku band

Frequency:  12573

Polarity:  Vertical

Symbol Rate 04444

FEC 1/2

In PAL

Reception Information for big dish (C Band) reception will be posted soon.

SOURCE: 

Friday, August 31, 2012

Facebook & Twitter Commentaries on Revelation

"Great news! I am ready to start the long-promised Facebook and Twitter Commentaries on the Book of Revelation on September 1 or shortly thereafter. The Facebook Commentary will involve the posting of one paragraph a day, working verse by verse through the Book of Revelation for however long it takes. I am guessing about five or six years. The Twitter Commentary will involve a Twitter length (less than 140 characters and spaces) summary of each day’s paragraph that will cumulatively provide a brief summary commentary on the whole book when it is done." - Jon Paulien at  http://revelation-armageddon.com/2012/08/30/my-new-commentary-on-revelation.aspx

Twitter: @JonPaulien

Wednesday, July 4, 2012

MARY WESEJA MIROBHO KUYENGA (1941 – 2012)



MARY WESEJA MIROBHO KUYENGA (Jan 01, 1941 – June 15, 2012)

Michael: “Nilizunguka Majita na hata Tanzania yote, na sikuweza kupata mchumba mwingine yeyote ambaye angenistahili, isipokuwa Mary Weseja Mirobho. Na hata kama ningeoa mwanamke mwingine awaye yote yule, asingeweza kustahimili dhoruba nilizozipitia mimi katika maisha. Tungeachana tu”. Ndivyo alivyosikika mgane Mchungaji mstaafu Joktan Muura Kuyenga, siku ya Jumamosi ya tarehe 16 Juni, 2012 akishuhudia jambo mojawapo alikumbukalo kumhusu marehemu mke wake, siku moja tu baada ya kifo chake.

Kazi za Maisha

Kulindwa: Mary Weseja Mirobho Kuyenga amekuwa mtumishi wa Mungu na mama mchungaji katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Tanzania na nje ya nchi pia. Baadhi ya kazi za utume huu mtakatifu ni pamoja na kuwa:
ü  Katibu muhtasi wa Askofu Mkuu wa Jimbo la Mashariki ya Tanzania (sasa Eastern Tanzania Conference)
ü  Katibu muhtasi wa Askofu Mkuu wa Jimbo la Kusini Magharibi mwa Tanzania (sasa Southern Highlands Conference)
ü  Kiongozi wa Shule ya Sabato Watoto na Vijana Watafuta-Njia chipukizi nchini India na Tanzania
ü  Kiongozi wa Chama cha Wake za Wachungaji katika Jimbo la Mashariki na pia Jimbo Kuu la Tanzania
ü  Katibu Muhtasi wa Idara ya Vijana ya Jimbo Kuu la Tanzania (Tanzania Union)
ü  Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Arusha, Tanzania, katika fani za Uhazili, hati-mkato, na Usimamizi wa Ofisi
ü  Mama halisi kwa vijana watatu na binti mmoja, wajukuu tisa, na vilevile mchungaji mwenza wa mumewe, yeye akiwa hodari kama mama-mchungaji.

Akishuhudia tabia yake kazini, mmoja wa mzazi-mwenza wa kike amemshuhudia kwa maneno haya, “Hata alipokuwa bado kijana, wakati tukiishi huko Majita, kamwe hukuweza kumsikia huyu mama akishutumiwa kwa masengenyo, ugomvi, wala zahama yoyote ile iliyokuwa ikisikika miongoni mwa wanawake wengine”. Na hivyo ndivyo alivyodumisha haiba yake. Aliendesha kazi zake kwa utulivu na busara, mara kwa mara akiimba wimbo: “Furaha na raha tutapata, Yesu anaporudi”. Utumishi huu ulidhihirika katika mikoa mbalimbali Tanzania, kila mahali akitia fora kama tai hodari arukaye katikati ya dhoruba.

Ndoa na Familia

Heri: Mary alichumbiwa kwa muda mrefu naye Mwinjilisti Joktan Muura Kuyenga. Haikudhaniwa na wasichana wenzake kama kweli Mary alikuwa na viwango alivyovitaka huyu Mwinjilisti “Joki”, kama alivyoitwa siku hizo, kutokana na ustaarabu wake wa kula ugali kwa kutumia uma (“masakiko”) na kisu. Japo Waswahili wasema fimbo ya mbali haiui nyoka, Mchungaji Kuyenga alimaliza masomo yake nchini Uganda, kisha hawa njiwa wawili wapendanao wakaunganishwa katika ndoa takatifu ya Ki-kristo tarehe 15 Januari, 1963 huko kwao binti, Iramba-Majita, mkoani Mara. Ndoa ilifungwa na hayati Mch. Daniel Mutani Yangwe. Miaka ya 1965, 1966, 1968 na 1971 walizaliwa kwao wana na binti, ambao wote walifuata nyayo za wazazi wao, na kuwa wachungaji katika Kanisa la Waadventista wa Sabato, naye binti kuolewa na mchungaji. Kuyathibitisha Maandiko Matakatifu ya Sulemani kuwa ya kweli, naam, hata kumhusu Mary Weseja Mirobho Kuyenga, “Wanawe huondoka na kumwita ‘Heri’; Mumewe naye humsifu na kusema, ‘Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote’” (Mithali 31:28-29). Isingalikuwa kunyakuliwa kwa mauti, Mary Na Joktan Kuyenga wangalisherehekea jubilei ya miaka 50 ya ndoa.

Chanzo cha Kifo

Deborah: Mchungaji Joktan Kuyenga, baada ya kushuhudia mateso apatayo mgonjwa wa kifua (asthma), alimsihi Mungu kwamba yeye atakapooa, aepushwe na mwenzi mwenye huo ugonjwa. Lakini Mungu si Athumani wala Yohane; muda mfupi sana baada tu ya kufunga ndoa, mwali wake alibanwa na kifua. Hata hivyo, kwa mkono wa BWANA na utaalamu wa utabibu, Mary alifanyiwa upasuaji kule Heri Mission Hospital, Kigoma, upasuaji ambao ulimpumzisha kabisa maradhi ya kubanwa kifua kwa muda wa miaka 40. Mwaka 2006 Mary aliibukiwa upya kwa mateso ya kifua, ambayo yaliibua pia masumbufu ya mapafu, vali ya moyo, figo, ini, na mirija ya uzazi. Katika hatua za mwishoni kabisa, ushauri wa utabibu uliondoa vilevile uwezekano wa upasuaji. Mary alipata ahueni fupi kwa kutumia madawa mbalimbali, hata hivyo miaka yake 70 ongeza mmoja aliyokuwa amepangiwa na Mwenyezi ilikuwa imetimia. Kwa utulivu wa matumaini tele ndani Yake Bwana na Mwokozi wake, Mary alipumua pumzi yake ya kutuaga, akiwa mikononi mwa binti wake wa pekee aliyekuwa tabibu wake nyumbani.

Hitimisho

Michael: Mary Weseja Mirobho Kuyenga ni jemadari aliyelala usingizi wa mauti. Baada ya mapambano makali lakini ya ushindi wenye kishindo kilichosikika mbinguni na akhera – shujaa, mama katika Israeli, amepumzika.
Ameweka silaha chini – shujaa hodari katika vita ya wema na uovu
Ameweka silaha chini – tai aliyetawala anga kwa ustadi wa mwanamke mchaji wa Mungu
Ameweka silaha chini – siyo kwa woga ama kukata tamaa, bali kwa kuipokea mede ya ushindi
Ameweka silaha chini – mama wa kweli katika Israeli
Ameweka silaha chini – ayala apendezaye, waridi la upendo halisi
Ameweka silaha chini – miguuni Pake Jemadari Mkuu Yesu Kristo aliyemuita ubavuni Mwake.
Ameweka silaha chini – hadi hapo tutapoisikia parapanda ya ufufuo!

Nasi leo twasherehekea kumbukumbu ya huyu hodari wa msalaba, tukilishangilia tumaini lile lenye baraka: “tazama Yuaja na mawingu, na kila jicho litamwona”, ndiyo, pamoja na lile la Mary Kuyenga.
Tuonane pale, Yesu Anaporudi.
-         
Imeandaliwa na Heri Gidion Kuyenga, Debora Nyamujungu Mang’ombe, Harun Kuliundwa Kuyenga, Michael Magesa Kuyenga.

Journal of Southern African Adventism (JOSA)

Dear Reader/Author/Friend,
 
It is with great pleasure to announce, on behalf of the editorial team, that the first issue of the online journal JOSA has just been published. It has indeed been an exciting journey, from conception to the first issue. We are however fully aware that this is just the beginning of a long and hopefully fruitful journey for all of us. The main purpose of JOSA is to provide a platform for knowledge sharing  as well as an arena for an informed conversation on issues that define what Adventism is and how it should find expression in Southern Africa. We hope this engagement will make the church more effective in its mission.
 
To access the papers/articles: 
- Please go to the website www.josa.co.za
- Click on the "CURRENT" tab at the top of the website
 
I assume you have registered as a reader (at least). If not, please go to the "REGISTER" tab (top of website) and follow the instructions. If you need help please contact us through the email address provided on the website or on this email address.
Because the first issue has now been published, we are likely going to get a good number of readers wanting to register and needing assistance with that and it might take a couple of days before we get to everyone who needs help.
 
We are already working on Issue No.2 (October 2012) and are calling for papers. Please think about writing.
 
Thanks for supporting JOSA and enjoy reading the papers.
 
God bless and Kind Regards
 
Alvin

Tuesday, May 8, 2012

Video za Angaza Kwaya Katika Tovuti ya Kanisa Manzese

Mtandao wa Maombi/Magomeni/Prayer Network



Mahojiano Kuhusu Historia ya Kanisa



Wajoli wa BWANA,

Ninawasalimu. 

Sabato ya jana ya tarehe 6,05,2012; nilibarikiwa sana kuabudu katika kanisa ambalo ni la kwanza kwa injili ya waadventista wasabato Ulimwenguni.

Nilialikwa na mwenyeji wangu ijumaa usiku ambaye aliniuliza kama ningekuwa radhi kwenda kusali kanisa la jirani. Nami sikusita maana huwa natamani kubadilisha mazingira, kama wengi wenu mnavyofanya. Ila sikufahamu kama kanisa tutakalokwenda, lina historia kubwa namna hii.

Tukiwa njiani siku ya sabato, alianza kunieleza historia ya kanisa hili, ambalo limeachwa kama makumbusho kwa historia ya kanisa letu. Nilipata raha sana kusali kanisa alilowahi kusali mama Elen White, teh teh! nikahisi kama napata upako mpya. hahaah!

Nimejaribu kuchukua picha chache za maeneo ya hapo kanisani, na pia nilimuuliza mmishenari mmoja wa kanisa letu la keene, ambaye kwa kweli anaifahamu historia vizuri. Nikapata wazo la kurekodi sauti yake wakati tayari tukiwa tumeanza mazungumzo. Nimeattach hiyo video. haiko organized vzr, na haina viwango vyenu kabisa ninakiri hilo nanyi mtashuhudia, lakini natumai mtabarikiwa kwa ujumbe.

Nilipata fursa ya kuona makaburi ya waumini wetu waliolala mauti 1907, 186..., (pichani kwa majina zaidi). 

kumradhi tena, Picha zimefifia kdg, ni kutokana na kifaa nilichotumia. Natumai mtabarikiwa ktk unyonge wake.

Tujiunge ktk viambatanishi  vyangu dhaifu.

Mbarikiwe

JRuby.

Tovuti ya Kanisa la Waadventista Wasabato Manzese

Tovuti ya Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania

Maranatha: Yesu Anakuja

Tuesday, March 27, 2012

SAFARI YENYE MATUMAINI

"Safari Yenye Matumaini"

Elias Wankyo

Isaya 43:18 "Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Tazama, nitatenda neno (jambo) jipya" "Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani."

New King James Version. Isaiah 43:18,19 "Do not remember the former things, nor consider the things of old. Behold, I will do a new thing" "I will even make a road in the wilderness and rivers in the desert."

Katika nchi ya Colombia kule Amerika ya Kusini mwanamke mmoja aitwaye Ingrid Betancourt aliamua kugombea Uraisi wa nchi hiyo. Katika mojawapo ya kampeni zake alitekwa nyara na kundi moja la ugaidi nchini humo. Kwa hali ngumu na ya kusikitisha alichukuliwa mateka na baadhi ya kundi lake na wakafichwa kwa muda wa miaka sita. Lakini mwaka 2008 mwishoni, Majeshi ya Serikali ya Colombia yalivamia maghaidi hao na kumkomboa Ingrid na watu wake wote wakiwa hai.

Ingrid aliporudi nyumbani salama alilakiwa na watu wakiwemo ndugu na jamaa zake. Ingrid akaenda mara moja kwa mama yake akamkumbatia kwa furaha iliyo kuu, na mbele ya waandishi wa habari akasema maneno haya mazito ambayo niliyaandika kuwa kumbukumbu nilipoyasikia kwenye taarifa ya habari:"Don't cry for me now. You don't have to cry for me anymore". Kwa Ingrid, inaonekana alikuwa tayari kufunga kitabu cha historia ya miaka 6 alipokuwa mateka, na kwa vile alikuwa huru sasa, alimwambia mama yake na watu wake, sasa kulia kwa ajili yake kungefikia mwisho, wafunge kitabu hicho kabisa, waanze maisha upya na waendelee na "Kitabu" kipya cha maisha.

1) Safari yenye matumaini inahitaji tusiwe watumwa (au kufungwa kama tuko jela) kwa uzoefu au mambo mabaya katika maisha yetu yaliyokwishapita. (Not to be prisoners of our negative "experiences" in the past).

Kila mwanadamu katika maisha amepitia hali fulani ngumu katika maisha, ila hali hizo zinatofautiana kati ya mtu na mtu. Kuna wengine ambao uzoefu au hali waliyopitia ni ngumu sana na imesababisha majeraha na makovu makubwa. Kwa sisi Waadventista tukikutana kanisani siku ya Sabato, hasa makanisa ya mijini, tumekuwa tumevaa vizuri, na kawaida tukiulizana, "habari gani?" Jibu la rahisi huwa kwa kawaida, "Ni nzuri". Lakini kwa ujumla tunaweza tusijue watu wanayopitia katikati ya wiki, au kwa ujumla katika maisha yao.

Nilikuwa katika mahubiri ya hadhara (Public Evangelism), Mhubiri alipotoa wito, nikashuka jukwaani, kuwapa mkono na kuwakaribisha walioitikia wito. Mama mmoja akasogea mbele akiwa na mnyororo mkubwa shingoni na mikononi. Nikamkaribia ili nijue alikuwa na nia gani. Kwa bahati mbaya hatukelewana kimazungumzo na hakuwa tayari kunisikiliza, ikabidi shemasi amchukue kwenda pembeni ya mkutano. Lakini suala hilo likawa kichwani mwangu kwa muda mrefu. Mfano mwingine, Sabato moja, niliomba watu walio na maombi maalumu waje ofisini kwangu baada ya ibada ili tuombe pamoja. Watu kadhaa walikuja. Mmoja wa waliokuja, alikuwa amempoteza mke wake kwa kifo mwaka uliokuwa umepita, na kipindi hicho, ndicho kilikuwa memorial anniversary.

Ilipofika zamu yake alisema, wiki hii nimekuwa nikitafakari kujiua kwa kumkumbuka mke wangu aliyefariki. Nilishikwa na mshangao mkubwa, ila nilificha moyoni mwangu kama kiongozi, ili nimpe matumaini na kuomba naye pamoja na kundi lililokuwa limekuja. Namshukuru Mungu kuwa Mzee huyo alipata matumaini kwa Bwana Mungu na aliendelea kuishi. Ninapotoa kisa hiki, ninakumbuka miaka yangu ya kuhudumu kule Texas miaka ya nyuma, lilikuwa ni kanisa dogo. Baadaye nikahamia State nyingine. Baada ya muda kadhaa, nikakutana na washiriki wawili kutoka kanisa lile dogo kule texas. wakanipa taarifa kuwa mama... mama fulani) alijiua. Nikaumia sana moyoni mwangu. Nikajiuliza, je nilipokuwa kule kuna jambo ambalo ningemsaidia huyo mama ambalo lingempa tumaini la kuishi. Je, katika mahubiri au mafundisho yangu ya Biblia, ni jambo gani ambalo ningelitoa ambalo lingemsaidia hata baada ya miaka kupita lingempa tumaini la maisha? Je, washiriki na viongozi wa kanisa hilo waliofuata, wangemsaidiaje huyo mama ili asifikie mahali na kukata tamaa ya kuishi?

Hali ya kukata tamaa sio ngeni. Tunakumbuka katika Agano la Kale kisa cha Musa alipotaka Mungu akatishe maisha yake, pia Nabii Eliya alipokuwa amekimbilia kwenye pango akiwa amekata tamaa ya maisha.

Kwa viongozi na washiriki wa Kanisa tuna majukumu makubwa, sio tu kwa ajili yetu wenyewe, bali pia na wale tunaokutana nao NDANI NA PIA NJE YA KANISA ili kujihimiza na pia kuwahimiza wengine ili kuendelea kuwa na matumaini kwa Mungu wa mbinguni katika safari ya maisha.

Mchungaji fulani katika conference fulani Amerika, alielezea kisa hiki kwenye mkutano wa Makambi: Alipokuwa Mchungaji kijana alitumwa kwenda kanisa fulani kuwa kiongozi hapo. Mara tu baada ya kufika mshiriki mmoja akaja kulalamika kuwa mwaka wa 1963 mshiriki mwingine alimtendea jambo baya sana. Huyu mchungaji kijana akasema, "Ndugu yangu suala hilo liliwatokea kabla ya mimi kuzaliwa. Sasa unategemeaje mimi nije kulisuluhisha, baada ya wewe kukaa nalo miaka hii yote na mko kanisa moja? Huyu mchungaji alitoa kisa hicho kufundisha umuhimu wa msamaha wa kikristo (forgiveness in Christianity).

Ni muhimu kusamehe na kuendelea na maisha mbele, La sivyo tukikaa na mabaya kwa muda mrefu, yanafanya madhara kwetu wenyewe kuliko wale tunaowakasirikia. Hata kama yule aliyetukosea asirudi kuomba msamaha, au asikubali kuongea ili kusuluhisha suala na misamaha itokee, jukumu letu ni kusamehe. Ila haya hayawezekani, isipokuwa kwa maombi na unyenyekevu tukimruhusu Roho Mtakatifu aendelee kufanya kazi mioyoni na akilini mwetu.
2)Safari yenye matumaini inahitaji tuwe na imani kwa Bwana Mungu wetu kwa ajili ya mapya.

Katika mafungu ya Isaya hapo juu, Bwana anaahidi kutufanyia kitu na/au mambo mema mapya.

Tunakumbuka yale Bwana aliyotutendea katika maisha yetu, lakini, tusiishie kwenye kumbukumbu tu (Memories only). Tumuombe Bwana ili kwa huruma na neema yake atusaidie tulio viumbe wake tumuone akitenda mapya makuu katika maisha yetu ya kila siku. Ni rahisi sana yule adui shetani kuleta vurugu na mawimbi, na giza, ili kujaribu kutuzuia tusione kazi ya Bwana ya kila siku katika maisha yetu.

Wakati fulani nilimsikiliza mhubiri aliyekuwa amealikwa kama Guest Speaker, ambaye alikuwa former, then retired, General Conference Executive Secretary. Pastor R. akasema kuwa alipokuwa katika uongozi no. 2 Executive position kule GC Headquarter, alichokuwa akisema au kufanya, in Official Capacity, kilikuwa kinapewa uzito mkubwa unaostahili. Ila mambo yalibadilika baada ya yeye kutoka hapo ambavyo ni kama kawaida kwa kila uongozi. Ila akasema kwa kusisitiza, hataki kukaa na kumbukumbu ya 'position' hiyo ya juu tu na kuacha kumfanyia Bwana kazi hali akiendelea kuishi. Pastor R. alieendelea, "The things we do for the Lord may not be written in the Adventist Review, other Church Journals, or even receive, "Thank You Notes" from others, but we must continue to do them, because we are doing for our Lord and Saviour Jesus Christ and His people". "Jesus has done a lot more for us. He gave His own life for our redemption".

3)Safari yenye matumaini inahitaji tumtumaini Bwana kwa ajili ya maisha yetu yajayo.

Yeremia 29:12. "Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho."

Katika mafungu ya Isaya 43:18-20 Bwana hakuahidi kuondoa misitu wala kuondoa majangwa katika maisha. Ila Mungu wetu ameahidi kuwa ataweka njia au barabara njema wakati misitu ikiendelea kuwepo, na ataweka maji mazuri wakati majangwa yakiendelea kuwepo.

As we travel through this New Year 2012, we have left the past, we are presenting our present, and committing our future in God's continued loving care, mercy, guidance, protection and the in-working of the Holy Spirit. In Him we live and move and have our being. "We have nothing to fear for the future, except as we shall forget the way the Lord has led us and His teachings in our past history" (EGW, Life Sketches, page 196).

Elias Wankyo

14 January 2012

THE PASSION OF THE GREAT COMMISSION


Tuesday, February 14, 2012

From Evolution to Creation: My Difficult Journey

From evolution to creation: My difficult journey

CONTINUE READING AT:

http://dialogue.adventist.org/articles/15_1_veith_e.htm

Thursday, February 9, 2012

BTYA Annual Winter Retreat Registration

Click this LINK to register

1. BTYA Annual Winter Retreat - March 2-4, 2012

Are we truly the body of Christ? How can we support others in their spiritual lives? Would you like to get to know your fellow young adults better?

Then join us for "Connecting the Dots: Strengthening the Body of Christ" with special guest speaker Pastor Orlando Hall.

Spend the weekend in peaceful Camp Winnekeag getting to know your fellow believers and learning how we can strengthen each other in our walks with Christ. Come grow closer to each other as we grow closer to him. Prices are as follows: Students - $35 / Non-Students - $45 / Saturday Only - $25 (Financial assistance available for those who need it). Registration is now officially open but will close on February 12.


Reserve your spot today! This will be a retreat you don't want to miss!

Sunday, January 29, 2012

MCHUNGAJI MBWANA ZIARANI MASSACHUSETTS

Mchungaji akiwahamasisha 'Tanzania Adventists in the United States (TA-US)'

Kwaya ya vijana wa TA-US wakiongoza uimbaji 'All Nations Church'

Saturday, January 21, 2012

Annual ACF//NAD Campus Ministry Conference

"The first annual ACF//NAD campus ministry conference will be held at Columbia University, NY April 13-15. College students from across the US, Canada, Bermuda and Guam will be gathering to celebrate a life in God on campus through worship, discussions, workshops and concert. Make plans to attend the first North American Division wide sponsored public campus ministry conference. For more info go to: www.acflink.org" - www.BostonCampusHope.org

GodEncounters for Young Adults (18-35)

"GodEncounters is coming up in just a couple of weeks (February 3-5) at Camp Winnekeag (257 Ashby Road, Ashburnham, MA). You can now register online (registration closes January 23rd) at http://auyouth.com/YoungAdults/god-encounters/!!" - www.BostonCampusHOPE.org